article Related Topics:
Luanda
 

Luanda (pia São Paulo de Luanda au Loanda) ni mji mkuu pia mji mkubwa wa Angola ikiwa na wakazi 2.776.125 (2005).

Jiografia


Mji wa Luanda uko mkoani Luanda kaskazini ya mdomo wa mto Cuanza mwambaoni ya Atlantiki.

Wakazi


Kati ya wakazi milioni 2,7 walio wengi kabisa ni Waafrika wa makabila kama vile Waovimbundu, Wakimbundu na Wakongo. Lugha rasmi ni Kireno lakini lugha nyingi za kibantu zinatumika pia.

Historia


Mji ulianzishwa mwaka 1575 BK na Wareno kwa jina la São Paulo de Luanda. Imekuwa mji mkuu wa Angola tangu 1627. Hadi 1850 Luanda ilikuwa kitovu cha biashara ya watumwa kwenda Brazil.

Wakati wa uhuru mwaka 1975 wakazi wengi Wareno waliondoka mjini. Vita ya wenyewe kwa wenyewe katika Angola kati ya 1974 - 2002 ilileta hasara pia kwa ajili ya mji mkuu.

Uchumi


Luanda ni bandari muhimu nchini pia mwanzo wa reli kwenda Malange.

Viungo vya nje


Miji Mikuu Afrika | Miji ya Angola | Angola

Luanda | Luanda | Luanda | Λουάντα | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | לואנדה | Luanda | Luanda | Luanda | ルアンダ | 루안다 | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | Луанда | Luanda | Luanda | Luanda | Luanda | 罗安达

 

This article is licensed under the GNU Free Documentation License. It uses material from the "Luanda".

Home Pageartsbusinesscomputersgameshealthhospitalshomekids & teensnewsphysiciansrecreationreferenceregionalscienceshoppingsocietysportsworld